Pages

Sunday, April 13, 2014

Breaking: Kuhusu mwanamuziki mkongwe mzee Gurumo kufariki dunia.

     Ni mzee wa siku nyingi sana kwenye muziki Tanzania ambae aliwahi kuingia kwenye vichwa vya habari mara nyingi hasa kutokana na kuugua kwake kuliko mfanya aache hata muziki aliokua anaufanya.


Taarifa zilizothibitishwa na hospitali ya Taifa Muhimbili kwa millardayo.com zimesema Mzee huyu amefariki dunia akiwa hospitalini hapo leo April 13 2014 saa nane mchana baada ya kuletwa jana asubuhi na kulazwa kwenye wodi namba 6 ya Mwaisela kutokana na kuzidiwa.

Tayari mwili wake umepelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti ambapo taarifa zaidi kuhusu chanzo cha kifo na taratibu za mazishi zitawajia hapo baadae

source: millardayo.com

No comments:

Post a Comment